30 November 2014


Kristina Pimenova mwenye umri wa miaka 9 ndio msichana mrembo kuliko woteduniani (!?) aliyechaguliwa mwaka huu.

Ni msichana mwenye umri wa miaka tisa kweli, na ili jambo limekuwa ndio sababu ya watu kuanza kujadili kama inafaa kuwa na watoto katika mambo ya urembo au la.

Kristina Pimenova mzaliwa wa Urusi, mwenye macho makubwa ya kibuluu ambayo kwa vigezo vya watu wa ulaya ndio macho yanayosemekana kuwa yenye kuvutia sana, ana midomo iliyokaa vema kama upinde na dimples ndogo pembeni mwa midomo yake.


Vitu hivyo pamoja na vigezo vingine ndio vimemfanya Kristina Pimenova mzaliwa wa Urusi kuchaguliwa kuwa binti mrembo kuliko wote. Zingatia kwamba vigezo hivi ni kwa watu wa Ulaya tu.

Kristina Pimenova amekuwa katika ulimwengu wa urembo tangia alipokuwa na miaka mitatu tu. Na amefanyakazi katika makampuni ya kutengeneza manukato kama vile Roberto Cavalli, Dolce & Gabbana na Armani.

Kwenye ukurasa wake wa Facebook, Kristina Pimenova ameandika kuwa anafurahiya sana kazi za urimbwende, hasa catwalk na maonyesho ya mitindo.


Ukweli kwamba kumekuwa na hali ambayo inatishia usalama wake na haswa ukizingatia commets zinazowekwa kwenye ukurasa wake wa facbook, ukurasa ambao una wafuatiliaji wasiopungua milioni mbili.

Wapo washabiki wake wanao muona kama ni msichana mrembo tu na wakimsifia hapa na pale na wakimtakia mafanikio kama msichana mdogo, lakini kuna wale ambao wana comment kwa viashilio vya ngono. Ambazo nyingi zimefutwa.

Comment nyingi ni za wanaume watu wazima wakiandika maneno kama vile "beautiful, I think I'm in love" na "marry me."


Hali kama hii imepelekea wazazi wake kuwa na wasiwasi picha zake zikachukuliwa kutoka kwenye mitandao na kutumika kwenye mitandao ya ngono.

Na vilevile kuna uwezekano wa Kristina kuja kunyanyasika kijinsia kama hatua za kiusalama hazita chukuliwa, na ili si kwake yeye tu, bali wa wasichana na wavulana wadogo wengi wenye kuhusishwa na biashara ya urembo duniani kote.

Je Msomaji una maoni gani kwa watoto wadogo kushirikishwa kwenye biashara ya Urembo na uonyeshaji wa mavazi na matangazo ya Mafuta ya Manukato!?

27 November 2014


Elimu ndio njia pekee ya kuwalinda wanawake na wasichana dhidi ya "kitendo cha kinyama cha ukeketaji" 

Wasichana na wanawake wengi Kaskazini mwa Tanzania wamefanyiwa ukeketaji unaofahamika kama tohara ya wanawake, kwa mujibu wa ripoti ya mwezi Juni 2013 iliyoandaliwa na Shirika la Watoto la Umoja wa Mataifa (UNICEF).

Utafiti huu umebaini mazingira ya kutisha kuhusiana na sababu zinazochangia ukeketaji. Pamoja na mila na desturi, umaskini pia umeibuka kama sababu inayozisukuma familia nyingi kukeketa watoto wao ziweze kujiongezea pato kiuchumi.

Mkoani Mara, kabila la Wakurya ndio wenye ukwasi mkubwa kutokana na ufugaji. Wakurya kwa upande wao, wameweka viwango vya aina ya mwanamke wanayetaka kumuoa. Kwa Wakurya mwanamke ambaye hajakeketwa, si mwanamke wa kuolewa. Kwa nia ya kuendeleza mila hizi, Wakurya wanatumia ukwasi wao kuongeza idadi ya ng’ombe wanaotolewa kama mahari kwa binti aliyekeketwa, hali inayoshawishi makabila mengine mkoani Mara kukeketa mabinti wao waweze kutolewa mahari kubwa na Wakurya.
Mikoa ambayo imekithiri sana kwa Ukeketaji ni, Mkoa wa Mara, mkoa wa Kilimanjaro, Ukiwemo Moshi na Arusha, Singida, Irangi na Dodoma.
Ingawa uungaji mkono wa mila hiyo unapungua, lakini kazi kubwa inahitajika katika kuelimisha jamii mbalimbali za kikabila.
Nchi za Kiafrika zinazo ongoza kwa Ukeketaji ni Misri, Ethiopia, Somalia, Djibouti na Nigeria ndizo nchi zenye idadi kubwa zaidi ya wanawake wanaofanyiwa ukeketaji.

Ukeketaji si mila ya kidini, ni kitendo cha kuogofya ambacho kwa ufupi ni unyanyasaji dhidi ya haki za kibinadamu za wasichana. Tuwe wazi kabisa, hili ni jambo ambalo halikubaliki kabisa na tendo ambalo linatakiwa liwe ni kinyume cha sheria za nchi, na linapaswa liwemo kwenye katiba ya nchi.

Ni wakati sasa wa kuongeza nguvu na kuelimisha wazee wa koo za kikabila kubadilisha mitazamo na kuwalinda wanawake nchini dhidi ya ukeketaji."

Tudhamirie haswa kukomesha tabia hii mbaya na isiyokubalika dhidi ya wasichana. 

Serikali ishirikiane na wanaharakati wa kijamii kupitia taasisi zake Kutoa elimu na njia mbadala za maisha kwa wafanyao ukeketeji na pia kushirikiana na viongozi wa kijamii kuhamasisha watu juu ya madhara ya muda mfupi na mrefu yanayosababishwa na ukeketaji.

Jeshi la polisi Tanzania limezindua mpango kazi wa miaka mitatu kupambana na unyanyasaji wa kijinsia na unyanyasaji wa watoto katika nchi, gazeti la Daily News la Tanzania liliripoti.

Waziri wa Mambo ya Ndani Emmanuel Nchimbi alitangaza mpango huo wakati wa Siku 16 za kampeni ya Harakati Dhidi ya Unyanyasaji wa Kijinsia, kampeni ya kimataifa inayolenga kuinua uelewa kuhusu suala hili.

Takribani asilimia 45 ya wakina mama wenye umri wa miaka kati ya 15 hadi 49 waliripoti kunyanyaswa kimwili au kijinsia katika maisha yao, kwa mujibu wa Utafiti wa Demografia na Afya nchini Tanzania wa mwaka 2010.

Watoto nao wako katika hatari kubwa, msichana mmoja kati ya watatu na mvulana mmoja kati ya saba wamenyanyaswa kijinsia, na zaidi ya asilimia 70 walinyanyaswa kijinsia kabla ya kufikisha umri wa miaka 18.

"Jeshi la polisi linawajibika kuboresha mwitikio wake kwa manusura wa [ukatili wa kijinsia] na unyanyasaji wa watoto," Inspekta Jenerali wa Polisi Said Mwema alisema.

Wakati huo huo ripota wetu anatuhabarisha kwamba, Serikali ya Tanzania imetoa mafunzo kwa maafisa 300 wa jeshi la polisi nchini kote katika juhudi za kukabiliana na unyanyasaji dhidi wa wanawake na watoto, Naibu Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba, Angellah Kairuki, aliliambia bunge siku ya Jumatano.

Miongoni mwa waliopewa mafunzo ya kushughulikia kesi za unyanyasaji wa kijinsia ni pamoja na maafisa 110 wa polisi, maafisa 110 wa magereza, mahakimu 60, madiwani 80 na pia viongozi wa kimila, kwa mujibu wa gazeti la Daily News la Tanzania.

Kairuki alisema Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora na taasisi nyengine pia zimechangia kwenye kujenga mwamko wa kushughulikia kesi za unyanyasaji wa kijinsia, na zimetoa mafunzo kwa maafisa tendaji wa wilaya katika mikoa 18 ya bara na mitano ya Zanzibar.

Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa tarehe 19 Februari, unyanyasaji wa kijinsia ni mkubwa sana Zanzibar ukiwa na kesi 996 na wa uko chini kabisa katika wilaya za Mara na Singida.

"Baada ya utafiti wa kina, imefahamika kwamba wanawake wengi katika maeneo ya vijijini yaliyo masikini wako kwenye hatari ya uwezekano wa kubakwa na aina nyengine za ghasia za kijinsia," alisema rais wa GG Trust, Stella Mathias. "Mafunzo haya yanakusudiwa kuwapa mbinu bora zaidi dhidi ya wabakaji."

Mathias alisema askari hao wa kike watawafundisha wanawake wengine mafunzo hayo ikiwa ni sehemu ya kampeni kubwa ya kuwafundisha asilimia 80 ya wanawake wa Tanzania namna ya kujilinda dhidi ya ghasia.

Ghasia zinazotokana na jinsia zimeongezeka katika baadhi ya maeneo ya Zanzibar na zimeendelea kuwa za juu katika maeneo mengi ya Tanzania, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa siku ya Jumatano (tarehe 19 Februari) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake cha Tanzania (TAMWA).

Katika kukusanya ripoti ya ghasia za kijinsia ya mwaka 2013, waandishi wa habari 30 wa Tanzania walikusanya data baada ya kupata mafunzo ya uandishi wa habari za uchunguzi kutoka kwa Shirika la Idadi ya Watu la Umoja wa Mataifa. Waandishi hao wa habari baadaye waliunda Mtandao wa Waandishi wa Habari dhidi ya Ghasia za Kijinsia.

"Matokeo ya utafiti wa siku kumi uliofanywa na waandishi hawa wa habari yamethibitisha bila shaka kwamba [ghasia za kijinsia] bado ni za kiwango cha juu nchini hii," alisema mjumbe wa bodi ya TAMWA, Gladness Hemed Munuo, katika uzinduzi wa ripoti hiyo jijini Dar es Salaam, kwa mujibu wa gazeti la Daily News la Tanzania.

Ripoti hiyo ilikusanya data za ubakaji, mimba za umri mdogo, ndoa za utotoni, utekelezwaji wa wanawake na watoto, na ghasia za majumbani katika wilaya tano za Zanzibar na 13 za bara, liliripoti gazeti la The Citizen la Tanzania.

Wachunguzi waligundua kwamba kiwango cha matukio kilikuwa cha juu visiwani Zanzibar kukiwa na visa 996, na kiwango kidogo zaidi kilikuwa kwenye wilaya za Mara na Singida. Katika utafiti wa mwisho, asilimia 20 ya wanawake wa Singida waliripoti kubakwa, lakini katika utafiti huu wa karibuni hakukuwa na kisa cha ubakaji kilichoripotiwa.

Vitendo vya ukatili vilivyopamba moto hivi karibuni vya mashambulio ya hadharani dhidi ya wakina mama kwa misingi ya nguo walizovaa, Wakenya wanatoa wito kwa hatua kali kuchukuliwa katika kudhibiti unyanyasaji wa kijinsia, ambao umeenea licha ya jitihada za kutunga sheria za kulinda haki za akina mama.

Unyanyasaji wa kimwili na mhemko unaendelea kuwa kero, pamoja na unyanyasaji wa kijinsia ambao umeripotiwa mara nyingi, kwa mujibu wa Kituo cha Kusaidia uponyaji unaotokana na Vurugu za Kijinsia (GVRC) katika Hospitali ya Wakina mama, ambayo hutoa tiba na msaada kwa manusura wa unyanyasaji wa kingono na nyumbani.

"Kati ya 2011 na 2012, jumla ya matukio ya unyanyasaji wa kijinsia 2,532 na matukio mengine 422 ya unyanyasaji wa kimwili uliripotiwa," Mkurugenzi Mtendaji wa GVRC Alberta Wambua aliiambia Sabahi.

Katika asilimia 90 ya matukio yote yaliyoripotiwa ya unyanyasaji wa kijinsia, wanawake na wasichana walikuwa waathirika, alisema.

Kituo hicho kimefanya majumuisho ya matukio 1,864 yaliyoripotiwa ya unyanyasaji dhidi ya wakina mama kati ya Januari na Mei mwaka huu, kukiwa na asilimia 84 ya matukio ya unyanyasaji wa kingono na asilimia 16 ya unyanyasaji wa kimwili, Wambua alisema.

Januari, kituo hiki kinatarajia kutoa ripoti kamili yenye matukio yote yaliyoripotiwa kati ya 2013 na 2014. Wambua alisema idadi ya jumla hadi sasa inaonyesha ongezeko kubwa la unyanyasaji wa kimwili na kingono dhidi ya wanawake.

"Idadi tunayotoa inawasilisha sehemu tu ya matukio halisi yanayotokea na kuripotiwa katika nchi yote, ambayo inaonyesha wakina mama na wasichana wanapata shida kubwa ya maumivu na mateso," alisema, akiongezea kwamba jitihada za kuwafanya wanaume watambue uhalifu wa unyanyasaji kama huo unaopaswa kuongezwa.

Uvaaji wangu, uchaguzi wangu

Wambua alisema ameshtushwa na mashambulio ya hadharani yaliyoenea ya hivi karibuni dhidi ya wanawake.

Katika matukio mbalimbali, wanawake wamekuwa wakishambuliwa na kuvuliwa nguo kwa nguvu mtaani kwa sababu ya namna walivyovaa, alisema, ambayo ni ishara ya kutisha kwamba ghasia ya kijinsia kwa sasa inajumuisha mashambulizi ya kuvamia mbali na unyanyasaji wa nyumbani na mashambulio ya kingono.

Mamia ya waandamanaji walitembea Nairobi tarehe 17 Novemba kupinga shambulio la mwanamke aliyevuliwa na kundi baada ya kudai kuwa sketi yake ilikuwa ya kubana sana na fupi sana.

Siku moja kabla ya mkusanyiko huo mkubwa, polisi waliwakamata wanaume zaidi ya dazeni kuhusiana na kumfanyia mwanamke katika shambulio linalofanana na hilo katika kituo cha basi cha Nairobi.

Mashambulio mengine mawili kama hayo yameripotiwa huko Mombasa na Nairobi katika siku za karibuni, na yamesababisha kukamatwa kwa angalau polisi mmoja.

Matukio haya, ambayo yalitokea mchana kabisa, yamechochea hasira za wananchi kote nchini Kenya.

Wakenya wameitaka mitandao ya kijamii kulaani ukatili wa kijinsia na kutoa wito wa kuheshimu uhuru wa wanawake kwa kutumia alama ya #NguoYanguChaguoLangu, huku mjadala mkali ukiendelea kwa vikali katika vyombo vya habari.

Baada ya kuandamana kutoka Uhuru Park hadi kituo cha basi cha Embassava kwenye barabara ya Accra, eneo la moja ya mashambulio, waandamanaji hao walielekea kwenye ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi David Kimaiyo kuwasilisha malalamiko yaliyotiwa saini.

Waandamanaji walitembea hadi Mahakama Kuu ya Kenya, ambako Mwanasheria Mkuu Willy Mutunga aliwapokea na kuahidi atawasilisha malalamiko kwenye Baraza la Taifa la Usimamizi wa Sheria, ambapo yeye ni mjumbe.

"Uvunjaji huu wa sheria ambapo tunawaona watu wakiwavamia wanawake ni kinyume na katiba," Mutunga alisema kwa kundi lililoshangilia. "Wanaume hao wanawapa wanaume wengine jina baya."

Wanawake wadai kupewa uhakika

Wale waliohudhuria mkutano huo, ambao uliandaliwa na kikundi cha Kilimani Mums, walilaani shambulio na kuiomba serikali kuwafikisha wakosaji katika vyombo vya sheria. Pia walidai kwamba viongozi wa kisiasa walaani hadharani matukio hayo na kuwahakikishia wanawake usalama wao.

"Ukweli kwamba shambulio la kutisha lilitokea mchana kweupe kwenye mtaa wenye shughuli nyingi katika mji mkuu bado hakukuwa na [ofisa] wa polisi hata mmoja katika eneo ili kusaidia wanawake walionyanyaswa kimwili na kihisia kunaacha maswali mengi kuhusiana na hali ya polisi yetu," alisema Koki Gatabaki, mwenye miaka 29, muigizaji anayekua.

Ukiukaji huo unapunguza mafanikio ambayo Kenya imeyapata katika kuhakikisha haki sawa kwa wanawake, aliiambia Sabahi. "Inasikitisha, matukio kama hayo yanatokea kwa sababu ya wachache ambao wanafanya uhalifu hawaadhibiwi."

Matukio ya hivi karibuni ya unyanyasaji na ukatili yana athari kubwa kwa kuwa ni "ishara ya uvunjaji wa sheria na kukosa uvumilivu katika nchi," alisema wakili mstaafu wa mahakama kuu Kariuki Muthe'ngi, mwenye miaka 65.

Katiba ya Kenya na mswada wa haki unahakikisha kwa uwazi haki za wanawake, alisema.

"Sheria ni kali lakini utekelezaji ni dhaifu au haupo kwa sababu vyombo vya kutekeleza sheria viko katika usingizi mzito na vinachukua hatua pale tu wakati hali haivumiliki baada ya maandamano au wakati wanapoagizwa na viongozi wa serikali," aliiambia Sabahi.

"Mfumo wa Sheria za Jinai nchini Kenya haujawezeshwa vya kutosha kuwalinda wanawake na ukatili wa kijinsia licha ya Sheria ya Makosa ya Kubaka ya mwaka 2006 iliyotungwa na bunge kwa sababu inakosa utekelezaji na utaratibu wa ufuatiliaji wa vyombo husika vya serikali ili kuhakikisha ufuataji wa sheria na katiba," alisema.

Wachunguzi wa polisi na waendesha mashtaka pia wanakosa mafunzo maalumu kuhusu utoaji wa Sheria ya Makosa ya Ngono, ambayo ni mojawapo ya sababu kuu inayochangia kiwango kikubwa cha kuachiwa huru katika kesi hizo wanaporipotiwa, aliongeza.

Ghasia ya kingono na kijinsia inatakiwa kusimamiwa na wanasheria wazoefu tu na sio waendesha mashtaka wa polisi, alisema, akiongeza kwamba polisi kwa sasa wanasimamia kesi hizi katika mahakama zilizo chini yao, ambazo zinafafanua kwa nini nyingi miongoni mwao zinatupwa nje na washukiwa kuachiwa huru.

Mkuu wa Idara ya Uchunguzi wa Makosa ya Jinai huko Nairobi Nicholas Kamwende aliiambia Sabahi kwamba kikosi kilichobobea cha polisi cha "kuzuia uvuaji nguo" kiliundwa kushughulikia kuibuka kwa mashambulio dhidi ya wanawake.

Alisema inspekta Jenerali wa polisi amechagua dazeni za wanawake kufanya kazi kwa kificho katika vituo vya mabasi na maeneo mengine ya umma na amewawezesha kwa rasilimalii zote zinazotakiwa kufanya kazi hiyo.

Kamwende pia aliwatia moyo wanawake ambao walikuwa waathirika wa mashambulio hayo kujitokeza katika kituo chochote cha polisi ili kuandikisha maelezo, ambayo yatasaidia katika uchunguzi na kukamatwa kwa wahalifu. Alisema polisii watachukulia taarifa yoyote inayotolewa kuwa siri.

Viongozi wa dini wazungumza

Kuibuka kwa ukatili dhidi ya wanawake ni suala kubwa na viongozi wa dini wanapaswa kujiandaa vizuri kushughulikia tatizo hilo, alisema Askofu Mark Kariuki, mchungaji mkuu wa Kanisa la Deliverance lililopo Nairobi.

Kariuki alitoa wito kwa Wakenya wote, akianza na viongozi wa kanisa, kutumia tukio la hivi karibuni la ukatili wa kijinsia kama kichocheo cha kuanza kuzungumza na kuzuia "uelewa wa ukatili wa kingono na wa majumbani ulioenea katika mikusanyiko yao."

"Kwa amani iliyopo ya jamii, utatuzi wa matukio ya ukatili wa kijinsia ni kushughulika na wanaume na wavulana kama washirika dhidi ya hilo," aliiambia Sabahi, akiongeza kwamba viongozi wa serikali na wa dini wanapaswa kushirikiana kuendesha kampeni za kuzuia ukatili kwa kuwalenga wanaume.

Mchungaji Murungi Igweta wa Kanisa la Trinity Baptist huko Nairobi aliunga mkono, akisema ukatili dhidi ya wanawake "unazuia mchango wao katika maendeleo ya taifa na hali nzuri ya familia zao."

Alisema ilikuwa bahati mbaya kwamba baadhi ya wanawake hawaungwi mkono katika makanisa yao wanapotafuta talaka au kutengana kutokana na hali ya kunyanyaswa kimwili. "Inaweza hata kuwa hali mbaya zaidi katika matukio ambapo mwatirika anatengwa na kanisa katika mazingira hayohayo," aliiambia Sabahi.

"Ukatili dhidi ya wanawake unapaswa kushughulikiwa kiundani katika kanisa na wanaume waliohusika," alisema.

Wale wanaofanya ghasia dhidi ya wanawake wanapaswa kuaibishwa katika jamii zao na kuadhibiwa katika mfumo wa kisheria, alisema Mohamud Abdilahi, imamu wa Msikiti wa Amani ulioko Mombasa.

Pamoja na kuwa tukio la uvuaji nguo linaweza kuzaa uovu, alisema, hii bado sio utetezi wa kufanya ukatili wa kimwili, na mwathirika hapaswi kulaumiwa kwa shambulio hilo.

"Ukatili dhidi ya wanawake unaendelea kuwepo kwasababu ya wanaume katika jamii ambao wanafanya ukatili na hawawajibishwi," aliiambia Sabahi, akitoa wito wa adhabu kali zaidi na utekelezaji mzuri wa sheria kama kizuizi.

23 November 2014

Katika pitapita yangu huko katika mitandao ya kijamii nimekutana na hizi picha.
Inafurahisha kuona hata watoto wadogo wanakemea huu Wizi, dhuluma inayofanywa na baadhi ya viongozi. 

Picha kwa hisani ya page ya bwana 
Inkhosi ya Makhosi

21 November 2014

Hii Habri tumeletewa na Mdada na akatuomba tuiweke hapa ili wanawake walioko kwenye ndoa na wale ambao hawapo kwenye ndoa wapate kujifunza na kuchukuwa taadhari.

---
Naitwa Josephina (Si jina lake) mnaweza kushangaa kwa kuamua kuiweka habari hii kwenye mitandao ya kijamii. Lakini kwa mapenzi yangu nimeamua kukiweka kisa hiki ambacho kimenikuta kiwe funzo kwa wadada wote watakao bahatika kukisoma.

Kwa miaka mitatu mfurulizo nimekuwa katika matatizo makubwa sana kwenye njia yangu ya uzazi. Nawashwa sana ukeni, hospitali walisema kuwa nasumbuliwa na fungus.

Nikawa natumia dawa za aina mbalimbali na kila dawa imekuwa haileti matumaini ya aina yoyote. Kila nikitumia dawa baada ya wiki tatizo linarudi pale pale.

Nimekuwa mtu wa kujikuna muda wote, uchi unawaka moto kwa kujikuna. Nimeendelea na tiba mpaka likaibuka tatizo lingine jipya, kila ninapofanya tendo ndoa napata maumivu ambayo hayaelezeki. Wakati mwingine mpaka naanza ku-bleed.

Nikaona nirudi hospitali kwa vipimo zaidi ili kujuwa kinacho nisumbuwa haswa ni nini. Nikapima vipimo vya kansa, na wakatoa kinyama ndani na kufanya vipimo.

Baada ya wiki mbili majibu yakatoka, wakasema hakuna kansa ya aina yoyote. Lakini ajabu tatizo likawa linazidi kuongezeka na sasa siwezi tena kufanya tendo la ndoa.

Baada ya uchunguzi wa kina madaktari wakagundua kuwa ndani ya uke kwenye mlango wa kizazi kuna wekundu mwingi sana, usio wa kawaida. Badala ya rangi ya pink. kumbe ile rangi nyekundu ni sehemu ambayo inashambuliwa sana na bacterial wasio sikia dawa.

Wakajaribu kupeleka dawa hapo kwenye hilo eneo lililoathirika bado ilishindikana kuwaua walikuwa bado wanaonekana wanashambulia.

Ikabidi madatari muhimbili waniulize jinsi ninavyofanya usafi katika uke wangu.

Nikabidi niwaeleze ukweli nilichokuwa nafanya...!

''Huwa najisafisha kwa kuingiza vidole ndani kisha najiingiza Asali niliyoipaka kwenye pamba. Naingiza ndani ukeni ili Uke uwe umebana. Na vitu vingine vingi kama wasichana wengi tunavyo shauriana (VIUNGA KUMA)."

Madaktari wakaniambia sababu ya matatizo yangu yamesababishwa na hivyo vitu, vikiwemo Asali na manukato mengine. Bakteria wote ambao ni walinzi nimewaua kwa kuweka hivyo vionjo. Na ndio maana uke wangu unashambuliwa sana na bacteria ambao hawasikii dawa.

Ndugu zangu makungwi wenzangu, leo hii nalia peke yangu nilikuwa nikiunga sana uke wangu kwa viungio na naingiza vidole vyenye kucha ndefu wakati mwingine nikiingiza mpaka sabuni ili kijisafisha.

Ili kuokoa maisha yangu Madktari wamesema ni lazima wanitoe kizazi changu, sababu nikiacha itageuka na kuwa kansa.

Hali yangu ni mbaya kwa kweli na mimi bado binti mdogo natolewa kizazi nikiwa na miaka 29 tu.

Natarajia hivi karibuni kufanyiwa operation ya kutolewa kizazi. Naomba sana mniweke katika sala zenu ili operation iende salama...!

Nawapenda wote!

20 November 2014

Mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la Tatu Ikoko mkazi wa Mwananyamala jijini Dar, hivi karibuni alifunga mtaa kwa kutembea bila nguo baada ya kumfumania mumewe akiwa na mwanamke mwingine.

Chanzo chetu cha kuaminika kilisema mwanamke huyo aliondoka nyumbani kwake usiku wa Ijumaa iliyopita na aliporejea asubuhi, alimkuta mwenzake akiwa na kigori mwingine ndani ndipo alipopagawa.

“Alitoka usiku mzima akarudi saa moja asubuhi akamkuta bwana’ke yuko na mwanamke mwingine ndani,  akaanzisha vurugu, akavua nguo na kubaki na kanga moja na kuanza kupita mtaani huku akisema nivue nisivue na watu wakawa wanamuitikia vua.

“Baada ya hapo tu watu wazima na mashosti zake  walimshika na kumsitiri, akaja bwana’ke akamchukua wakaenda nyumbani kwao,” kilisema chanzo hicho.
Chanzo kiliendelea kufunguka kuwa tukio hilo siyo mara ya kwanza kwa mwanamke huyo kwani alishawahi kufanya hivyo akiwa na mwanamume mwingine aliyejulikana kama Kisiso mtaani hapo na waliachana kwa tabia hiyo.

“Akiwa na mwanaume halafu akamfumania, ndiyo huwa anafanya hivi na yule mshikaji wa kwanza kwa aibu ilibidi ahame, sasa hivi anaishi Mbagala,” kilisema chanzo hicho.

Imeletwaa na Shani Ramadhani & Mayasa Mariwata.

19 November 2014




"My grandchildren are dead there for years. Somehow forgot me death "

Mahashta Mûrasi is an Indian who claims to be born in 1835. It is not only the oldest man in the world but. also the man who lived the longest since the history of mankind (according to the Guinness World Records ).


According to the information transmitted, the man was born in Bangalore on January 6 1835.De 1903, he lived in Varanasi, where he worked until 1957, until his retirement in 122 years.


According WorldNewsDailyReport.com all official documents to identify this man support his version


My grandchildren have died there a few years, "said Mûrasi." In a way, death has forgotten me. And now I have lost all hope to die! "

17 November 2014

  • Bwana Harusi Amwacha bibi Harusi Kwenye Sherehe ya harusi yao baada ya kuona uso wake kwa mara ya kwanza wakati mpiga picha aliwataka wapozi kwa ajili ya picha
  • Harusi hiyo iliyofanyika Magharibi mwa mji wa Madinah.
  • Maharusi hawakuwahi kukutana uso kwa uso kabla ya sherehe ya Harusi
  • Wewe si yule msichana ambaye nilikuwa nikimfikiria... sina budi nikuache'
  • Mwanamke mwingine uko uko Saudia amepewa talaka kwa kutojibu mesei ya whatsaApp alotumiwa na mumewe.
Bwana Harusi Amwacha bibi Harusi Kwenye Sherehe ya harusi yao baada ya kuona uso wake kwa mara ya kwanza wakati mpiga picha aliwataka wapozi kwa ajili ya picha.

Mwnamume wa Kisaudia amemweleza Bi Harusi kuwa amempa talaka Mke wake mpya siku ya harusi yao, baada ya kuona uso wake kwa mara ya kwanza wakati mpiga picha alipowataka wapozi kwa ajili ya picha.

Harusi hiyo iliyofanyika Magharibi mwa mji wa Madinah. Iliingia kitimu timu baada ya bwana harusi kuona uso wa Bi harusi na kutamka hayo aliyoyatamka.

Maharusi hao hawakuwahi kukutana uso kwa uso kabla ya sherehe hiyo wala kuona picha za kila mmoja wao.

Kizaa zaa kilianza pale tu, Bi Harusi aliponyayua veli lake uku akitabasamu kwa dhumuni la kupiga picha za ukumbusho, ndipo bwana Harusi hakaruka kimanga na kutamka kwa hasira uku akisema kwa sauti kubwa '...Wewe si yule msichana ambaye nilikuwa nikimfikiria. Utanisamehe, Nasikitika ila sina budi nikuache... Nimekuacha'
Hivi karibuni kuna mwanamke mwingine uko uko Saudia ambaye amepewa talaka kwa sababu tu, akuweza kujibu mesei ya whatsaApp alotumiwa na mumewe.
Baada ya kuondoa veri uku akitabasamu kwa ajili ya kamera, mume haliruka na kusimama ghafla kwa miguu yake uku akisema kwa hasira, ...Wewe si yule msichana ambaye nilikuwa nikimfikiria. Utanisamehe, Nasikitika ila sina budi nikuache... Nimekuacha'

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Okaz, bi harusi ghafla naye aliangua kilio cha machozi kwa mshituko alioupata na kuzimia. Jitihada za ndugu na jamaa hazikuweza kutatua wala kusuruhisha tatizo lililojitokeza.

'Bwana harusi alisema hakuwahi kuona uso bi harusi kabla ya ndoa'

Furaha ya harusi kwa ndugu, jamaa na marafiki iliingia doa na kugubwikwa na machozi ya uzuni badala ya vicheko, nderemo na vifijo 'Wakati bi harusi alipo tamkiwa tu kuwa ameachwa kwa sababu sura yake haikumvutia bwana harusi. Na ndipo bi harusi alipo anguka na kupoteza fahamu.

Mmoja wa waandishi katika mitandao ya kijamii  aliandika kuwa, Bwana harusi amefanya jambo baya na lisilo kubalika katika jamii: 'Amemsababishia mwenzake maumivu makubwa maishani mwake kwa kuwa tu na mtizamo wa kibinafsi na uchoyo wa nafsi, akifikiria kuwa uzuri wa mwanamke ni sura na si tabia.

'Kwa bahati mbaya, vijana wengi wa sasa wanacho angalia wao ni uzuri wa nje au umbo la mwanamke na si tabia wala maadili.

'May God give her a better husband who will appreciate her for who and what she is.

15 November 2014

Huyu ndie mhitimu bora wa chuo kikuu cha UDSM mwaka 2014,anaitwa Doreen Kabuche ana miaka (22) alitangazwa kuwa kinara wa ufaulu kwa kupata alama 'A' 32 na B+ 6 kati ya masomo 38 ya shahada ya Takwimu Bima(Actuarial Science)

Kwa alama hizo Doreen Kabuche alipata wastani wa alama Za ufaulu (GPA) 4.8 na kuacha alama 0.2 ili kufikia kiwango cha juu kabisa cha ufaulu wa alama 5.

Doreen alimaliza elimu yake ya sekondari mwaka 2008 katika shule ya forodhani na alifanikiwa kupata division one  ya point 9,akachaguliwa kujiunga na shule ya sekondari ya  Benjamini Mkapa

Akichukua mchepuo wa EGM  na ndiye aliyekuwa msichana wa kwanza kitaifa kwenye mtihani wa necta kidato cha sita kwa kupata div one ya point 4. 

Hongera sana Doreen wewe ni mfano wa kuigwa


12 November 2014

MWANDISHI wa gazeti la Jamboleo kutoka mkoani Iringa Bw Francis Godwin ameteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa chama cha Wamiliki Mitandao ya Kijamii (Blogs) nchini Tanzania.

Godwin ambae ni mmiliki wa blog ya "MatukioDaima" na "FrancisGodwin" ameteuliwa katika nafasi hiyo kama mwakilishi wa wamiliki wote wa blogs za mikoani, huku Joachim Mushi akiteuliwa kuwa mwenyekiti wa chama hicho.

Uteuzi huo umefanyika leo katika ukumbi wa Mlimani City baada ya kumalizaka kwa warsha ya siku moja iliyoandaliwa na mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA).
Wengine walioteuliwa ni pamoja na Katibu wa chama hicho Khadija Kalili, ambapo wajumbe ni Mdimu Henry, William Malecela, Othman Maulid na Shamim Mwasha.

Akizungumza mara baada ya uteuzi huo mwenyekiti wa chama hicho Bw Mushi alisema kuwa lengo ni kuhakikisha katiba ya chama hicho inakamilika mapema zaidi ili chama hicho kiweze kusajiliwa rasmi.

Mkurugenzi mkuu wa TCRA, Profesa John Nkoma alisema kuwa mamlaka yake itasaidia kufanikisha mchakato mzima wa wamiliki wote wa blog nchini kuwa na chama chao na kuwa lengo ni kuwawezesha kufanya maamuzi yao kwa umoja na kuweza kusimamiana wenyewe.

Profesa Nkoma alisema kuwa iwapo wamiliki wa blogs nchini wataanzisha chama chao upo uwezekano mkubwa wa TCRA kuwasaidia mchakato huo na pia kuendelea kuungana na chama hicho kwa kuendelea kutoa elimu zaidi.

Mbali ya kuwataka kuanzisha chama hicho,  bado aliwataka wamiliki wa blog nchini kuendelea kuifanya kazi hiyo kwa kuheshimu misingi ya maadili badala ya kutumia vyombo hivyo kuvuruga maadili.

Akielezea kuhusu uwajibikaji wa blogs nchini kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, alitaka kuhakikisha wanatoa nafasi sawa kwa vyama na wagombea wote bila upendeleo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa idara ya habari (Maelezo) Assah Mwambene aliwataka wanahabari nchini na walimiki wa blogs kuendelea kuutumia vyema uhuru wa vyombo vya habari na kuangalia mambo ya msingi kwa jamii badala ya kugeuza mitandao hiyo kuvuruga amani ya nchi.

Safu ya Uongozi:

  • Mwenyekiti: Joachim Mushi
  • Makamu Mwenyekiti: Francis Godwin
  • Katibu: Khadija Kalili
  • Wajumbe: Shamim Mwasha, Mdimu Henry, William Malecela, Othman Maulid

11 November 2014

By Kichaa Cha Mwendawazimu Aliyechanganyikiwa

%^&*()+£€?# zenu....! Leo nahisi Kichaa changu kimepanda au sijui kimepandishwa, yaani hata sielewi, kinacho endelea vichwani mwa Wabongo wanaoishi ndani ya nchi ya Wachawi Giningi, heri mie Mwendawazimu Kichaa Aliyechanganyikiwa, kwa sababu hakuna anayeweza kuniangalia mara mbili, zaidi ya wale watoto wanaopenda kunitania na wengine wakifikiria kuwa eti nimesoma sana mpaka vitabu vikiniona vinachakaa vyenyewe, ndio akili zikaelewa saaaana mpaka nikawa Mwendawazimu Aliyechanganyikiwa.

Hivi hawa wenye akili sana zilizopitiliza mpaka wakawa Wachawi, uwa wanafikiria nini kwenye vichwa vyao, hivi hawajui kuwa wale wenye akili robo ndio walio wachaguwa kuwa pale walipo? Eti nasikia kuwa baadhi ya vyama vya Kichawi vimeamua kuungana ili kukichangia na kukigomea chama Kikuu cha Wachawi.

Ah ah ah ah ah...! Kaaazi kweli kweli...! Wachawi awa awa si ndio kwenye Bunge lao la Wachawi, wamejipandishia masurufu kiasi cha kutisha, kama kweli hawa Wachawi wapo kule kutetea Misukule na Mandondocha, wangekuwa wanawashirikisha ndondocha na misukule wote kabla ya maamuzi yao. Lakini ni pale tu, Chama Kuu la Wachawi, likitumia uchawi wake mkuu, ndio utawaona Wanga na Wachawi wengine wakipiga kelele na kucheza mahepe, wakitaka kuwashirikisha ndondocha na misukule.

Nao Mandondocha na Misukule kwa kulewa na Uchawi na Urozi wa vyama vyao vya Kichawi wanawashabikia, wamelewa dawa za kuondoa akili a.k.a propaganda kiasi ya kwamba hawaoni hawasikii.  Ushabiki umekuwa mkubwa kiasi ya kwamba hawaoni wala hawasikii tena. Wanatamanishwa kila leo, lakini masikini hakuna wanacho kipata, wanaomba, wanatamani, mwisho tamaa na maombi yanasahaulika.

Wachawi wote, lao moja, sioni hata Mchawi mmoja mwenye afadhali. Sasa hivi kila kona unayokwenda Misukule na Mandondocha wanalalamika hali ngumu! Utamkuta mtu jicho limemtoka  kama yai la Mbuni "Hatukubali. Ngoja uchaguzi uje. Mchawi huyu sasa basi. Mimi kura yangu kwa naniu tu safari hii. Eeh, ndio! Mffvyyyy! Kshxnz$!!! kabisa! Blah...blah...blah...!"

 Ukiwa Mwendawazimu Aliyechanganyikiwa kama mimi ndio unafaidi. Miye sina Mchawi hata mmoja ninaye mpenda. Usiniulize, kwa sababu Kichaa haulizwi, ukitaka kuwauliza bora uwaulize hao hao Misukule wenzio au waulize Mandondocha, ndio wenye uwezo, japokuwa hawajui kuwa wana uwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko ya maisha yao.

Nauliza tu wale wanaojidai wana hasira, hasira hizo ni za kweli au Vifuko vikitolewa tu, "Thalamaleku, uku wengine bwana athifiwe nyiiingi...!"

Wengi wanashangaa haswa lengo la haya ninayoyasema ni nini, wacha niwaambie kuwa sina lengo lolote, kwanza toka lini Mwendawazimu Aliyechanganyikiwa akawa na malengo? Hayo malengo muwe nayo nyinyi wenye Akili na Wachawi wenu walio wafanya nyinyi kuwa Mandondocha na Misukule, mnalishwa pumba sawa! Mkilishwa Makapi sawa! Ila mkimwa matumbo, mkienda uko mnapo paita Sipiti-ni-hatari, I mean Sipatihali, Oops nina maanisha Hosipitali, ndio hosipitali, mnakumbana na maudhi mengine na kukatishana tamaa.

Hakuna Mafusho ya kufukisha wala, hirizi za kuwavika msiumwe magonjwa ya kuhara, matumbo yanasokota kwa kula pumba kavu, sasa unashangaa nini, kwani tangu lini, ndondocha au msukule akatibiwa?

Basi wacha niwaambie na nina uhakika kabisa Wandondocha na Misukule wote wamekwisha hukumiwa kifo tayari...! Ndio kwani hujui kuwa Bongoland, hukumu ya kifo inafanyakazi!?
Ndio inafanyakazi japokuwa si kwenye mahakama rasmi, lakini Wachawi wakishirikiana na Wanga wamesha wahukumu... Japokuwa si kile kifo cha kunyongwa hadi kufa kwa kuning'inizwa kambani au kupigwa risasi lakini cha moto wanakiona...! Maana wanakufa taratibu wakijiona na machozi yenda na maji hakuna wa kuyaona.

Tena siku hizi wachawi hawa wenye akili sana wamehamia Mbinguniiii kwa taarifa yenu. Maana hata kujenga wanajenga uko uko mbinguni, uku ardhini wanakuja tu, siku za Ijumaa na Jumapili, ili nao waonekane onekane, ili hali wanajuwa kuwa Mungu wao na Mungu wa Mandondocha ni tofauti.

Uko Sipiti-ni-hatari, I mean sipitali wanaotibiwa ni Wanga na Wachawi wenye kujiweza kidogo, kwa sababu, wao ndio Wabia wa nchi hii. Ila wale Manguli wa Uchawi walio na Ubia katika nchi hii... Unashangaa nini, ndio kwani hujui kuwa nnji hii imikwisha uzwa, shauri yako... Basi Wachawi wakipata faida, upeleka kuweka pesa zao uko mbinguni Uswisi. Wakitaka kufanya shopingi za wajukuu zao wanao wandaa kuja kutawala Ndondocha, wanakwenda zao mbinguni Dubai, mapumziko mbinguni Ufaransa, wakiumwa haoooo wenda zao mbingu ndogo India, ila Wachawi wengi wanaona kuwa mbingu ndogo India siku hizi hata baadhi ya Mandondocha wanakwenda, basi tena wamebadirisha, wenda zao Mbingu ya Londoni na wengini mbinguni Marikani.

Lakini ni ajabu sana Wachawi hawa, matibabu, shopingi, mapumziko yooooote yanafanyika Mbinguni, basi na mkifa Mzikwe uko uko Mbinguni, muwaambie jamaa zenu kabisaaaa, maana Bongoland sio Makaburini.

Ndioo... Eeeeh, Haiwezekani Mtumie mapesa yoote kwenye kujifaharisha uko Mbinguni, siku mkikata roho tu, mnaletwa duniani (Bongoland) kuja Kuzikwa, kwani mmesikia kuwa Bongoland ndio Makaburini, kwanini msizikwe uko uko Mbinguni kwenu!?

9 November 2014



Miss Tanzania namba mbili,ambaye sasa anachukua nafasi ya kwanza Lilian kamaziama anatatizo la kiuraia.
Hili ni kutokana na baba wa mrembo huyo jenerali kamaziama kuwa na msuguano kuhusu uraia wake,hivyo itaturudisha Kule Kule kuwa mrembo huyu Tanzania Asili yake ni mnyarwanda

"Hili Taji la mrembo wa Tanzania wahusika wangefumba macho apewe Lundenga mwenyewe tumechoka alooo"
Nimekutana na komenti hizo katika pita pita zangu leo hii katika mitandao ya kijamii nikasema wabongo shikamooni,sasa huyu mnyarwanda Yule namba tatu si ndio mrangirangi kabisa kazi ipo.
Lilian kaza buti vizuri upokee kijiti ulichoachiwa na mrembo aliyeng'atuka bi Sitti.
Ujiandae vyema na maswali ya wana habari,sio ukajijibie tu Kama upo katika vibaraza vya wapiga soga, fahamu watanzania wanakujua kuliko wewe unavyojijua yap hii ndio sifa kubwa ya wabongo kujua ya watu kuliko ya kwako kwa hiyo chunga sana.
Jus sasa watakuwa wameshafatilia vyeti vyako vya kuzaliwa ,wameshajumlisha kiwango chako cha elimu na miaka yako,wameshajua kuwa wewe sio Mtu wa Arusha,lakini ulikwenda shiriki huko na mengi mengineyo.
Usijali kuhusu uraia kwani Tanzania inamachotara kibao ha ha ha ha ha ha ha.
Kila la kheri katika kuiwakilisha Tanzania huko katika shindano la dunia.
Nimemaliza.

7 November 2014





THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

TANZANIA COMMUNICATIONS REGULATORY AUTHORITY


ISO 9001:2008 CERTIFIED

TAARIFA KWA UMMA

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA INAPENDA KUWATANGAZIA WAMILIKI WOTE WA MITANDAO YA KIJAMII “BLOGERS” KUWA KUTAKUWA NA MKUTANO TAREHE 11.11.2014 KUANZIA SAA TATU ASUBUHI UKUMBI WA MLIMANI CITY JIJINI DAR ES SALAAM.

MKUTANO HUO UTAJADILI MATUMIZI YA BLOGS KIPINDI CHA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA WABUNGE NA RAIS KAMA ILIVYOAINISWA KWENYE RASIMU YA MWONGOZO WA MAUDHUI KWA AJILI YA KAMPENI ZA UCHAGUZI MWAKA 2015.

TAFADHALI MNAOMBWA KUFIKA BILA KUKOSA.

Imetolewana
MkurugenziMkuu
MamlakayaMawasiliano Tanzania
S.L.P. 474
DAR ES SALAAM
https://www.tcra.go.tz

6 November 2014

 
 

IRINGA, Mwanamke mmoja mjini Iringa amtupa mtoto wake chooni mara baada ya kumzaa nyumbani.

Mama mmoja mjni Iringa anayetambuliwa kwa jina la Magdalena Limano mwenye umri wa miaka32, amemtupa mtoto wake chooni mara baada ya kumzaa.

 

Mshukiwa

Mtoto huyo wa kiume alizaliwa tarehe 4/11/2014 majira ya jioni na mama huyo na kuamua kumdumbukiza chooni, sababu alizotoa ni kwamba, kuna uwezekano mkubwa kuwa mtoto huyo si wa mume wake wa ndoa.

Mume wa mwanamke huyo yupo safarini kikazi na hana taarifa zozote za ujauzito wala taarifa za mke wake kujifungua na kitoto kuupwa chooni.


Chanzo cha habari kinasema kuwa, Magdalena uwa na tabia ya kumdanganya mumewe na kutoka na mabwana wengine pindi mumewe akiwa safarini kikazi.

Mtoto huyo aliyetupwa choon majira ya jioni mara baada ya kuzaliwa na kukutwa asubuhi ya tarehe 5/11 asubuhi akiwa analia ndani ya choo na majirani na kutoa taarifa.

Kwa juhudi za wasamalia wema, waliweza kumuokoa kichanga icho na kwa sasa mtoto ni mzima wa afya tele na yupo katika uangalizi mzuri wa hospitali huku mama yake mzazi akishikiliwa na jeshi la polisi akisubiri kufikishwamahakamani, kujibu shitaka la kujaribu kuuwa mtoto wake wa kumzaa mwenyewe.

2 November 2014








Thousands Attend Anti-Water Charge Protests in Cork City & County

Protests under the Right2Water in Cork city and towns in the county including Bandon, Clonakilty, Fermoy, Cobh, Mallow and Youghal.

In the past two weeks, the Anti-Austerity Alliance and the People’s Convention have organised protests in Cork city which have each attracted about 1,000 people.

The protest takes place in the Grand Parade on Satardays

.

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!