25 February 2016


Unapoingia kwenye majumba ya waislam wengi si jambo la kushangaza kukuta Luninga  (TV) varandani na wakati mwingine mpaka vyumbani, kwenye vyumba vya kulala.

Watoto wetu wa siku hizi wamekuwa kama mazombi (mandondocha), hawana utulivu tena na luninga ndio imekuwa kibembelezi kwa watoto wanao tusumbua au kulia lia pale tunapokuwa na maongezi au jambo ambalo linaitaji usikivu.

Lakini hali hii si kwa watoto tu, hata watu wazima, maana hao ndio kabisa wamekuwa mandondocha (Zombies), unaweza kumkuta mtu anashangalia TV hata habari hana, swala zinampita, majukumu yake ndani ya nyumba yanampita, yeye yupo kakodolea macho michezo ya tamthilia, mashindano ya  mpira na michezo mingine isiyo na maadili, yaani luninga ndio zimekuwa Qibla kipya kwa Waislam wa karne hii.

Watu wengi ujiona hawajakamilika kama ndani ya nyumba hakuna Luninga na ujiona kama washamba au hawajaendelea, sababu tu hakuna Qibla kipya cha kukielekea.

Ile hali ya kuishi kifamilia ndani ya nyumba miaka hii imepotea kabisa, watoto hawachezi tena nje, wakitoka nje basi wanataka kuiga yale walio ona kwenye luninga, wazazi nao hawapo nyuma, fasheni za mitindo ya mavazi filamu na tamthilia kwenye luninga ndio zimekuwa masimulizi ya kila siku kwenye simu na mazungumzo ya kawaida wanapo kutana.

Wataalam wa saikolojia wanatuambia kuwa Mtu mzima/mtoto anayetumia saa tatu na zaidi kwenye luninga kila siku kuna uwezekano wa kupoteza utulivu na umakini darasani au katika kazi zake. Na hii inasababishwa na ile michezo inayotolewa kwenye vipindi vya luninga na kuchota mawazo na akili kiasi cha kusababisha pumbao na ustarehevu wa muda kwenye akili ya binadamu.

Na inapotokea mtu au mtoto kukosa zile pumbao, basi akili yake inakosa utulivu na ujiona mchovu na upoteza hali ya uchangamvu na umakini katika jambo analotaka kulifanya.

Sina maana ya kuwakataza watu wasitazame Luninga lah hasha, tunaweza kutazama haswa kama vipindi vitakuwa na mafundisho na faida kwetu na haswa vipindi vya dini, taarifa za habari na vipindi vya kimaendeleo nakadharika.

Lakini tutakapoigeuza Luninga (TV) kuwa ndio Qibla chetu, hapo ndio tutakuwa tumepotea na kukipoteza kizazi chetu, maana tutakuwa tunaangalia kila kinachojili kwenye luninga, kiwe chenye maadili au lah. Na kisha tunashangaa kuwa watoto zetu wana tabia za ajabu ajabu na tunashangaa wapi wamezipata, kumbe ni kile Qibla kipya tulicho kinunua kwa pesa nyingi na kukitafutia nafasi nzuri varandani kwetu.

Unatarajia Mtoto/Watoto Watakusikiliza Kweli Wakati Katuni wanazo Tazama Ni Hizi...!

• Tarzan: Maisha yote anaishi Nusu UCHI
• Cinderella: (Kisonoko) kila leo anakirudi nyumbani usiku wa manane.
• Pinokio: UONGO wakati wote.
• Aladdin: ni MFALME WA WEZI.
• Batman: anaendesha gari mbio kwa Mwendo kasi wa 200 mph.
• Romeo & Juliet: WALIJIUWA Kwa Sababu ya MAPENZI.
• Harry Potter: Anatumia UCHAWI.
• Mickey & Minnie: Ni zaidi ya MARAFIKI.
• Sleeping Beauty: Msichana MVIVU.
• Dumbo: Ni MLEVI.
• Scooby Doo: Kla siku yeye na Ndoto za MAJINAMIZI.
• Snow White: ANAISHI NA WANAUME SABA Chumba kimoja.

Hatupaswi Kushangaa Wanapokosa ADABU. Kwa sababu wanajifunza Tabia na Mienendo kutoka kwenye vipindi vya katuni kwenye Luninga na Vitabu vya hadithi za Watoto, ambavyo maadili yake hayaendani na Uislam.

Tunapaswa badala yake kuwa kuwafundisha simulizi za Maswahaba wa Mtume (saw) kama vile:

• Abu Bakr (ra) alivyokuwa ni Muaminifu, Kweli na Muadilifu.
• Umar ibn Khatthab (ra) Uvumilivu, Upendo kwa ajili ya kutetea HAKI.
• Uthman ibn Affan (ra), Haya na Staha.
• Ali ibn Abi Talib (ra) Ujasiri na Ushujaa.
• Khalid ibn Waleed (ra) Tamaa ya kupambana na Maovu.
• Fatima bint Muhammad (ra) Upendo na Heshima kwa baba yake.
• Sallahuddin Al-Ayubi (rh) Shujaa aliye Ikomboa Jerusalem.

Na Mengine Mengi Mazuri kutoka Kwente Historia (Tarekhe) ya Kislam...
Zaidi ya yote...

Tunapaswa kuwafundisha juu ya kumpwekesha MwenyeziMungu (swt), Kusoma Qur'an na Sunnah za Bwana Mtume (saw).

14 January 2016

Kuwa na harufu mbaya mdomoni ni kitendo kinachoweza kuathiri maisha ya mtu kimahusiano si kwa mpenzi tu bali marafiki na jamii kwa ujumla. Pia kuwa na harufu mbaya mdomoni uondoa haiba ya kupendwa kwani hata unapoongea wengi watakwepa kuongea moja kwa moja na wewe kwa sababu ya harufu mbaya inayotoka mdomoni mwako.

Chakula unachokula kina athiri hewa inayotoka mdomoni au sehemu nyingine za mwili wako. Baadhi ya vyakula vina matokeo mabaya sana kwa hurufu unayotoa mdomoni. Harufu mbaya mdomoni si ugonjwa wa kuambukiza haina haja kuogopa ukikutana na mtu mwenye harufu mbaya mdomoni kwamba atakuambukiza.

Pia tatizo kubwa ni kwamba watu wenye harufu mbaya mdomoni hawajijui kwamba wana harufu mbaya. Asilimia 85 - 90% ya tatizo la harufu mbaya mdomoni asili yake ni kinywa chenyewe. Pia kiwango cha harufu hutofautiana kutokana na muda (mchana, usiku na asubuhi).

Harufu nyingi mbaya mdomoni hutokana na vyakula vyenye asilia ya protein. Kuna zaidi ya aina 600 ya bacteria wanaoishi kwenye kinywa cha Binadamu (sehemu ya juu ya ulimi, fizi na kuzunguka meno).

KINACHO SABABISHA HARUFU MBAYA MDOMONI

Kutokuwa makini na usafi wa kinywa kama vile kupiga mswaki vizuri kunakoacha mabaki ya chakula ambayo huoza na kusababisha harufu mbaya mdomoni. (Wengi hupiga mswaki haraka haraka na kuacha mabaki ya chakula). Maambukizi ya magonjwa kama vile fizi kutoka damu, mfumo wa upumuaji na kisukari. Kinywa kuwa kikavu kutokana na madawa (medications) Kuvuta sigara, kunywa kahawa, ulaji wa vyakula vyenye viungo vikali kama vile vitunguu maji au thaumu.

NAMNA YA KUJUA KAMA UNA HARUFU MBAYA MDOMONI

Wanasayansi wamekiri kwamba ni ngumu sana mtu kujijua mwenyewe kama ana harufu mbaya kwa sababu ya mazoea (habituation).
Ni rahisi sana kutambua harufu kutoka kwenye kinywa cha mtu mwingine. Unaweza kutambua kama una harufu mbaya mdomoni kwa kumuuliza mtu unayemuamini.
Pia unaweza kujua harufu mbaya kwa kulamba nyuma ya kiganja na kunusa, wengine hupumua mbele ya kioo na kunusa. Pia unaweza kutumia kijiti cha kuchokonolea meno na kukinusa. Kisayansi unaweza kutumia vifaa kama Halimeter, Gas Chromatography na BANA Test.

NAMNA YA KUJILINDA NA HARUFU MBAYA MDOMONI (TIBA) 

Kula vyakula vyenye afya na vyakula ambavyo wakati unakula vinaweza kusafisha kinywa vizuri. Kusafisha meno mara kwa mara au kwa uchache mara mbili kwa siku asubuhi na baada ya mlo wa usiku, hii usaidia kuondoa au kujikinga na harufu mbaya mdomoni. Vilevile unashauriwa kutumia KISAFISHA ULIMI (tongue cleaner) kusafishia ulimi wako. Tumia bazooka (chewing gum) ambazo husaidia kuongeza kiasi cha mate kwenye kimywa kilichokauka. Baadhi ya gums zina viungo vinavyoondoa harufu mbaya mdomoni na zingine husafisha kinywa na bacteria wanaosababisha harufu mbaya. Tumia dawa ya kusukutua mdomoni (mouthwash) kabla ya kulala usiku. Kuwa makini na afya ya kichwa chako kama vile kupiga mswaki vizuri, kuondoa mabaki ya vyakula kwenye meno na kumuona daktari kila unapoona una Matatizo ya meno au kinywa au kila baada ya miezi sita kwa uchache.
Kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha kila siku angalau glass mbili za maji.
Mwone daktari wako ukiona una tatizo la harufu mbaya mdomoni.

NAMNA YA KUJIKINGA NA KUONDOA HARUFU MBAYA MDOMONI!

Watu wengi husumbuliwa na tatizo la kunuka mdomo bila hata kujijua hivyo kuwa kero kwa wenzao na wakati mwingine hujishushia hadhi mbele ya jamii. Mara nyingi ugonjwa wa kunuka mdomo (Halitosis) husababishwa na uchafu wa kinywa na ulaji wa vyakula usiosahihi lakini ni tatizo linalotibika.

Ni rahisi kulizuia na kuliondoa tatizo la kunuka mdomo iwapo utaamua kufuata kanuni za usafi wa kinywa na unywaji wa maji kwa kufuata kwa makini muongozo ufuatao:

KUPIGA MSWAKI

Kitu cha kwanza kufanya ni kupiga mswaki kwa ukamilifu kila uamkapo asubuhi. Wakati wa kupiga mswaki, utatakiwa siyo tu kusugua meno, bali pia ulimi, sehemu ya katikati hadi karibu na koromeo kwa kusugua vizuri. 
Vile vile kila uamkapo baada ya kulala mchana au jioni, hakikisha unapiga mswaki, kwani bakteria wa kinywani, hutawala kinywa kila ulalapo. Mara baada ya kupiga mswaki na kusugua ulimi sawaswa, hakikisha unasukutua vizuri kwa maji, kwani hapa ndipo baadhi ya watu hukosea kwa kupiga mswaki bila kusukutua kwa maji.

KUNYWA MAJI MENGI

Maji ni muhimu sana karibu kila eneo la mwili wa binadamu. Unywaji wa maji ya kutosha kila siku utakusaidia kudhibiti na hatimaye kuondoa tatizo la kunuka mdomo. Unywaji wa maji mengi ni muhimu, hasa kwa wale watu wenye ugonjwa wa kukauka midomo (xerostomia).

Mara nyingi harufu itokayo mdomoni, hutokea tumboni na siyo kinywaji peke yake kama unavyoweza kudhani. Hivyo, kama tumbo litakuwa chafu, hata kama utasafisha kinywa vizuri bado harufu mbaya inaweza kuendelea kutoka. Harufu mbaya ya tumboni hutokea pale tumbo linapokuwa chafu kutokana na kutopata choo kwa muda mrefu. Miongoni mwa mambo yanayochangia kukosekana kwa choo kwa muda mrefu ni pamoja na tabia ya kutokunywa maji ya kutosha kwa siku, hivyo hakikisha unakunywa maji, kiasi kisichopungua lita moja na nusu hadi mbili au zaidi, kutegemeana na kazi unazozifanya.

Ukiwa na tatizo la kukaukiwa maji mwilini kila mara, mwili hujaribu kutumia njia zake za kiasili kupunguza uzalishaji wa mate ili kuhifadhi maji kwa ajiili ya matumizi mengine, kitendo hicho huchangia kunukisha mdomo kwa sababu ndani ya mate huwa kuna kinga muhimu dhidi ya baktetria wanaonukisha kinywa.

Kwa upande mwingine, ili kuzuia kinywa kunuka pale mdomo unapokuwa umekaukiwa na mate, ni vizuri kutafuna vitu kama bazooka (chewing gum) yoyote ili kuzalisha mate ambayo huhitajika katika kudhibiti bakteria.

MWISHO:

Hakikisha unasukutua sawaswa baada ya kula chakula chochote, hata kama ni juisi isipokuwa unapokunywa maji tu ya kawaida. Bila shaka, ukizingatia haya, tatizo ulilonalo la kunuka mdomo litataoweka na kubaki historia.


18 September 2015

Kambi Maarufu ya wahamiaji na wakimbizi, mjini Calais, nchini Ufaransa yenye kujulikana kwa jina la THE JUNGLE.


Hii ni Kambi ya Wahamiaji na Wakimbizi iliyopo Mjini Calais, Ufaransa.

Wengi wao ni kutoka Eritrea, Ethiopia, Libya, Afghanistan, Iran, Iraq, Sudan na Syria

"Kila aliyeko kwenye kambi hii mjini Calais si kwamba anapenda au anataka kuishi hapo Calais la hasha. Kila mtu aliyepo hapo ndoto yake ni kwenda kuishi nchini Uingereza."


Takriban watu 4,000 wanaishi katika kambi karibu na bandari ya mji wa Calais. Idadi kubwa ni vijana, lakini pia kuna wanawake wachache na watoto. Wengi wao ni kutoka Eritrea, Ethiopia, Libya, Afghanistan, Iran, Iraq, Sudan na wakimbizi kadhaa wanatoka nchini Syria.


Wote wamesafiri kwa muda wa wiki au miezi kadhaa au hata miaka wakizunguka nchi za Ulaya kwa lengo la kufika Calais, ambayo ipo maili zisizo pungua 30 kutoka mkondo wa bahari ya Waingereza kuelekea Uingereza (English Channel).

Hali ya kambi, si nzuri kabisa kwa binadamu yoyote kuishi humo.

Kambi imezungukwa na dampo, kiasi cha kusababisha matatizo ya kiafya kwa wakazi wake. Magonjwa kama vile ukurutu (Upele) ni jambo la kawaida – magonjwa yamacho na maambukizi ya kuumwa kifua unaosababishwa na vumbi na mchanga.


Na nje ya Kambi kuna uzio ambao una ncha kali na polisi wakipokezana ili kuwazuiya wale wote ambao watajaribu kuingia eneo ambalo magari makubwa yameegeshwa kusubiria zamu ya kuingia kwenye shimo au handaki ambalo linapita chini ya bahari kuanzia Ufaransa mpaka Nchini Uingereza.



Kuna mashirika yasiyopungua matatu na baadhi ya watu binafsi ambao wanajaribu kwa njia moja au nyingine kuwasaidia wahamiaji hao na wakimbizi waliopo hapo kambini.

Mara chache chache ukiwa ni mkaazi wa hapo unaweza kupata hema la kulalia, blanketi na hata vyakula vya kwenye makopo.


Wakazi wengi ambao wamejaribu kuingia Uingereza kwa kuruka uzio wa waya zenye ncha kazi wamejikuta wakijeruiwa aidha na waya zenye ncha kali au kupigwa na polisi wa ufaransa. Wapo ambao wamejikuta wakiumizwa na malori ya mizigo na hata kupoteza maisha.

26 July 2015

Individual consumers can show their opposition to Israel’s Apartheid policies against the Palestinian people and violations of international law by participating in a consumer boycott of Israeli goods and services. A boycott can also put pressure on companies whose exports are linked to some of the most evident aspects of the Israeli occupation and apartheid.















22 July 2015


Msahafu huo Unaweza kuwa ndio mkongwe zaidi duniani unapatikana katika Chuo Kikuu cha Birmingham, nchini Uingereza.

Baada ya vipimo vya kujua umri wa vitu mbalimbali ‘Radiocarbon dating’ kuonyesha kuwa umri wa Msahafu huo ni miaka isiyopungua 1,370, hii inapelekea msahafu huo kuwa miongoni mwa msahafu mkongwe kuwepo duniani katika asili yake.

Msahafu huo ambao umeifadhiwa kwenye maktaba ya chuo kikuu cha Birmingham kwa karne moja tangia ulipoletwa na kuifadhiwa kama moja ya miswada ya ukusanyaji wa vitabu na nyaraka za kutoka Mashariki ya Kati, bila kutambuliwa kuwa ni moja ya azina kongwe kabisa katika ulimwengu wa Kiislam.
Mshafu huu uligunduliwa kuwa mkongwe baada ya mtafiti wa shahada ya uzamifu (PhD), Bwana Alba Fedeli, alipoamua kufanya uchunguzi wa karibu zaidi katika kurasa za huo msahafu na kuzifanyia vipimo kwa kutumia mionzi yenye kujua au kukisia asili na umri viumbe mbalimbali (Radiocarbon Dating) na matokeo yalikuwa ni ya kushangaza sana.

Mkurugenzi chuo hicho cha makusanyo ya vitu maalum, Susan Worrall, alisema watafiti awakutarajia wala kuota kuwa msahafu huo utakuwa ni wenye umri huo. Na kuwa wao wamepata bahati ya kuwa na kopi ya asili ya Msahafu ambao unasadikiwa uliandikwa kipindi cha Makhalifa.

Vipimo, vilivyofanywa na Chuo Kikuu cha Oxford Radiocarbon Accelerator Unit, vilionyesha kuwa msahafu huo, umeandikwa kwa kutumia aidha ngozi ya kondoo au mbuzi, na ni miongoni mwa maandishi makongwe sana ya Qur’an kubakia katika asili yake.


Vipimo hivyo vimeonyesha kuwa uwezekano wa tarehe ni zaidi ya asilimia 95%, kuwa uliandikwa kati ya mwaka 568 na 645.

Profesa David Thomas, wa Chuo Kikuu cha Birmingham, amesema kwamba...
Mtu ambaye ameandika kwa kweli kabisa atakuwa anamjuwa vizuri Mtume Muhammad... atakuwa amemsikia akihubiri... Msahafu huo unatupeleka kipindi cha miaka michache ya mwanzilishi halisi wa Uislamu," 

"Kwa mujibu wa historia ya Kiislamu, Mtume Muhammad alipata ufunuo ambao ndio umekusanywa na kuwa Qur’an, kati ya mwaka 610 na 632, mwaka ambao alifariki."

Prof Thomas anasema kuwa mwandishi wa nakala ya msahafu huo inawezekana kabisa alikuwa ni mmoja wa maswahaba ambao wamemuona Mtume Muhammad (saw). Mtu ambaye atakuwa anamjuwa vizuri Mtume Muhammad, na atakuwa pia amemsikia akihubiri na atakuwa ni mtu wa karibu kabisa na Mtume (saw).

Source: 'Oldest' Koran fragments found

17 July 2015


Assalamu Alaikum Wa Rahmatu Allah Wa Barakatuh

'Iydul-Fitwr Al-Mubaarak
Taqabbala Allaahu Minnaa wa Minkum


Kwa Munaasabah huu wa furaha wa siku hii tukufu ya ‘Iyd Al-Fitwr tunapenda kuchukua fursa hii kuwawasilishia salaam zetu za siku hii na du'aa njema kwenu wote, tukimuomba Allah (Subhaanahu Wa Ta'ala) Atutaqabalie 'amali zetu na zenu ‘TAQABBALA ALLAAHU MINNAA WA MINKUM’ (Hivi ndivyo Maswahaba watukufu walivyokuwa wakiambiana pindi wanapokutana katika siku ya 'Iyd). Na tunamuomba Yeye Aliyetukuka na Mweza, Awajaalie furaha, amani, mapenzi, siha na Iymaan pamoja na karama na utukufu katika masiku yote ya uhai wetu.

Mwisho, bila kuwasahau wenzetu katika du'aa zetu leo na kila siku. Ndugu zetu Waislam waliopo palipokuwa Qiblah cha kwanza cha Uislam, na Msikiti wa tatu kwa utukufu na hadhi, Palestina hasa walioko Gaza. Na wengineo walio katika dhiki za ukandamizwaji, vita, njaa na machafuko popote walipo Waislamu ulimwenguni.
Tunamuomba Allah (Subhaanahu Wa Ta'ala) Atutakabalie du'aa zetu na za Waislam wote duniani, Aamiyn

22 June 2015


Bakwata leo uko wilayani Bagamoyo walikuwa kwenye mchakato wa kumpata mrithi wa kukaimu nafasi ya Muft/Sheikh Mkuu wa Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mohamed Mhinga, alisema Baraza la Ulamaa litakaa na kuteua kiongozi atakayekaimu nafasi hiyo kwa muda siku 90 kabla ya kufanyika uchaguzi.

Na leo wametimiza ahadi hiyo kwa kumchaguwa Sheikh Abubakar Zubeir kukaimu nafasi hiyo ya Muft, atakaekaimu kwa muda wa siku 90 huku wakiendelea na utaratibu wa kufanya uchaguzi mkuu wa kumchagua Muft.

Uchaguzi huo utafanyika baada siku 90 kumalizika na fomu za kugombea zitatolewa kwa wagombea ambao watatoka miongoni mwa Baraza la Ulamaa ambao watachujwa mpaka kubaki mmoja.

MASHEIKH WA BAKWATA WENYE UWEZO NA WA KUMRITHI:
Baraza la Ulamaa ambalo ndilo litakalotoa Sheikh Mkuu mpya wa Tanzania linaundwa na Kadhi Mkuu, Sheikh Abdallah Mnyasi na manaibu wake, Sheikh Abubakar Zubeir na Sheikh Ali Muhidin Mkoyogole.

Wengine ni  Sheikh wa Mkoa wa Mwanza, Salum Fereji, Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga, Ismail Makusanya, Sheikh wa Mkoa wa Kigoma, Hassan Kiburwa na Kadhi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Hamid Masoud Jongo.

Sheikh Abubakar Zubeir, amechanguliwa leo uko wilayani Bagamoyo, atakaimu nafasi ya Muft Mkuu kwa siku tisini (90) kisha watapiga kura kumchagua nani anafaa kuchukuwa nafasi hiyo.

HABARI MPYA
Habari tulizozipata muda si mrefu zinasema kuwa "Mchakato wa kumpata Sheikh Mkuu utakamilika ndani ya siku saba (7) kuanzia sasa, wananchi na waumini wa dini ya kiislam na haswa wanachama wa BAKWATA wawe wavumilivu katika kipindi hiki," alisema Sheikh Lolila.

Katibu mkuu huyo hakutaka kuweka wazi sehemu wanapokutana wajumbe wa Baraza la Ulamaa ambao ndilo lenye mamlaka ya kumchagua kiongozi.

Sheikh Abubakary Zubery

Habari tulizozipata hivi punde zinasema kuwa Sheikh Abubakary Zubery amechaguliwa kuwa kaimu Mufti katika uchaguzi uliofanyika Bagamoyo,Sheikh Zubery alizoa kura zote zilizopigwa. 

Baadae wataongea na waandishi wa habari, kwa ufafanuzi zaidi.





15 June 2015


Habari zilizotufikia muda si mrefu ni kwamba Mufti Mkuu wa Tanzania Shekh Issa Shabani Simba Amefariki dunia, leo asubuhi.

Mufti Shekh Issa Shabani Simba, alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya Kisukari kwa muda mrefu kidogo. Kabla ya kufariki, Marehemu Muft Simba alikuwa amelazwa kwenye Hospitali ya TMJ Mikocheni na alikuwa amefanyiwa operasheni ndogo kabla ya umauti kumkuta.

Taarifa ya mazishi kwa mujibu wa Sheikh wa mkoa Alhadi kupitia Radio Quran yatafanyika siku ya Alhamisi, Mkoani Shinyanga.

Kwa wale wote watakaopata nafasi basi wanaweza kuudhuria Msibani nyumbani kwake Mikocheni, jijini Dar es Salaam.

--DUA'A
Ewe Mwenyezi Mungu  hakika Issa Shabani Simba yuko katika dhima yako na kamba ya ujirani wako, basi mkinge na fitina ya kaburi na adhabu ya moto nawe ndiwe mstahiki wa utekelezaji na ukweli, basi msamehe na umrehemu hakika Wewe ni mwingi wa kusamehe, mwingi wa kurehemu.

Aamiyn

2 June 2015

Hii ni moja ya video iliyo rekodiwa na mwana dada Hoyce Temu, video hii imepigwa maeneo ya Tandika, Wilaya ya Temeke Mkoa wa Dar es Salaam.

Mtangazaji huyu aliweza kuwatembelea watumiaji wa madawa ya kulevya na kushuhudia jinsi wanavyo jidunga sindano, kwa kutafuta mishipa ya damu, haswa maeneo ya mikononi na miguuni. Na ikishindikana kupatikana basi ufikia hata kujidunga kwenye maeneo ya shingoni ambako mishipa ya damu ipo karibu sana na Moyo na wenyewe wanakiri kuwa ni hatari na dawa upanda kwa haraka zaidi.

Wachache walio hojiwa wanaomba kama ikiwezekana basi wapatiwe msaada ili waweze kuacha kutumia haya madawa.

Je wewe una maoni gani kwa watumiaji wa madawa ya kulevya, je unao uwezo wa kuwatembelea maeneo yao na kuwapa ushauri nasaha au kuwaelekeza maeneo ambayo wanaweza kupata msaada ili waepukane na haya matumizi ya madawa ya kulevya!?

Video hapa chini inajieleza.


27 May 2015


Taarifa zilizo tufikia ni kwamba, Muigizaji Maarufu wa Radio na Television, Bi Catherine Mapunda, Maarufu kwa Jina la Uigizaji Bi Nyakomba, amefariki dunia.

Marehemu Bi Nyakomba alipata umaarufu katika michezo ya maigizo redioni wakati huo ikirushwa na Redio Tanzania (RTD) akishirikiana na wasanii wenzake wakiwemo Hamisi Tajiri al maarufu Meneja, Ibrahim Raha al maarufu Mzee Jongo, Bakari Mbelemba al maarufu Mzee Jangala, Mzee Kagunga, Mzee Majengo na wengine,


Amefariki katika hospitali ya Jeshi la Polisi katika barabara ya Kilwa, alikopelekwa usiku wa kuamkia tarehe 25 May 2015 baada ya kuzidiwa.

Bi Nyakomba alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari tangia mwaka 2012.

Marehemu Bi Nyakomba amezikwa tarehe 26 May 2015 saa tisa alasiri kwenye makaburi ya Chang'ombe jijini Dar es Salaam baada ya ibada ya mazishi iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Maurus, Kurasini.

Ndugu wa familia ya marehemu wamesema Bi Nyakomba amefariki akiwa na umri wa miaka 64 akiacha watoto sita na wajukuu kumi na watatu.



Enzi za uhai wake, Channel TEN iliwahi kufika katika nyumba yake huko Keko Juu katika Kata ya Mburahati, Manispaa ya Temeke ili kumjulia hali wakati akiugua pamoja na mambo mengine, alihusia wasanii hususan vijana kote nchini, kuifanya sanaa kwa nidhamu kwa kuwa ni kazi rasmi kama kazi nyinginezo.

Blog ya tmark-turn inawapa pole na mkono wa rambirambi kwa ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote na wapenda sanaa kwa ujumla.



6 May 2015

An Indian court has sentenced Bollywood star Salman Khan to five years in jail for killing a homeless man in a 2002 hit-and-run driving incident in Mumbai.

The man was among five people who were run over in the incident. The actor was charged with culpable homicide.

Khan had said his driver was behind the wheel, but the judge said the actor was driving the car and was under the influence of alcohol at the time.

Legal experts expect the actor to appeal against the verdict.

He could have been jailed for 10 years.

But correspondents say the guilty verdict is a huge setback for Khan who is one of Bollywood's biggest stars, appearing in more than 80 Hindi-language films.

Salman Khan
The actor is one of Bollywood's most bankable stars
Crowd outside Salman Khan's house
Many fans and onlookers gathered outside his house in Mumbai

Several of his films, including Dabangg, Ready, Bodyguard, Ek Tha Tiger, Maine Pyar Kiya and Hum Aap Ke Hain Kaun, have been huge commercial hits.

On Wednesday morning, as the actor drove to court with his family and friends, fans prayed for the actor's acquittal.

But Judge DW Deshpande found him guilty on the charge of culpable homicide.

"You were driving the car; you were under the influence of alcohol," he told the actor as soon as the court proceedings began.

Indian television channels reported the actor broke down inside court as the guilty verdict was announced.

Several of his Bollywood colleagues spoke out in his support and expressed their sympathies. Actress Hema Malini said she was praying for him and hoped he would escape with a light sentence.

If the actor is jailed, it will affect several big-ticket film projects he is involved in at the moment.

Driver's testimony

The case has gripped Bollywood and India for years.

Late on the night of 28 September 2002, Khan's Toyota Land Cruiser hit the American Express bakery in the Bandra area of Mumbai, authorities say.

The vehicle ran over five people sleeping on the street, killing 38-year-old Noor Ullah Khan and seriously injuring three others. Another person received minor injuries.

The prosecution alleged that Khan had been driving the car while drunk, both of which charges the actor denied in court in March.

But many witnesses disagreed.

A constable attached to Khan's security detail said in a statement to the police that the "drunk" actor had lost control of the car. The policeman died in 2007 of tuberculosis.

In April, Khan's driver told the court that he had crashed the car after a tyre burst but the court did not accept that version.

Grey line

Case timeline

September 2002: Salman Khan's car runs over five people sleeping on a Mumbai street, killing a homeless man and injuring four others

October 2002: Khan charged with culpable homicide not amounting to murder - arrested but granted bail

May 2003: Court rejects his plea to drop culpable homicide charge

June 2003: Bombay high court drops culpable homicide charge; actor is then tried for rash and negligent driving

October 2007: Prime witness, a constable who served in his security detail, dies

March 2015: Khan tells the court he was not drunk and his driver was behind the wheel

May 2015: Khan found guilty, sent to jail for five years



18 April 2015


Glamour World and Food Section..... Get best of your day from Primacla 
Decorations & Catering. 
Get a different best day look by decorating with PRIMACLA and make your day perfectly great in your wedding,birthdays,sendoff, anniversary,kitchen party,baptism and even in funeral ceremony.  






In Decor and catering Primacla treats you peculiar. Contact: +255754710600+255659468484+2557672444000, email: fnkya57@gmail.com
Insta: faithnkyaberege

.

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!