22 August 2014

Nimeipata hii sehemu kwa kweli nimeipenda Kama na wewe utapenda chukua huu ushauri.
Binafsi nilisha anza kuwaweka pembeni hao watu basic people ha ha ha ha

Hivi ndivyo alivyoanza....

Kuna baadhi ya LEVEL huwezi kufika...Kuna MAFANIKIO huwezi kuyafikia...Kuna HELA huwezi kuzipata...Kama umezungukwa na watu BASIC...
Kuanzia asubuhi mpaka jioni wanaongelea WATU TU..Fulani kamegwa na yule..halafu yule naniliu sasa hivi anatembea na yule ex wa nanii...Asubuhi mpaka jioni DISCUSSING PEOPLE...

Hawa ndio watu BASIC...Hata siku moja hawatakupa Ushauri kuhusu HOW TO REACH SOMEWHERE...NEVER
Na ukionekana unaanza kufanya vitu EPIC watakugeuka kwamba UNARINGA..UNAJISIKIA..UMEWATENGA...UNAJIDAI UNA HELA...and lots of bullshit...

Pengine ulipaswa kuwa mbaaalii kibiashara lakini HUWEZI sababu umezungukwa n Mbaazi tupu...BASIC PEOPLE...Ukiwaambia umesikia Kiwanja kinauzwa Kigamboni wanakwambia Kigamboni watu wanatapeliwa kuna mradi wa Joji Bushi...Ukiwambia unataka kujiunga Forever Living wanakwambia UNALIWA HELA...Ukiwaambia kuna SACCOSS wanatoa mikopo unataka uchukue ujenge wanakwambia INTEREST ZAKE UTASHINDWA na kujenga sio mchezo shosti..Unaamini unaacha!...Nataka kufanya Kitu flani WANAKUKATISHA TAMAA

Unahitaji kuzungukwa na watu wenye POSITIVE ENERGY ambao ukiwambia unataka kwenda Mbinguni kwa kupitia Mkuranga wanakuchangia Nauli...Niliposema naacha kazi watu ohh utakula nini..utaishije...Mji Mgumu huu..Wenzio wanatafuta kazi we unaacha utalosti...

WHO SAID??Nadunda kama kawa..Subaru inatembea kama kawa na Business zinaenda kama kawa...NEGATIVE PEOPLE WILL BRING U DOWN....Ukitaka Kupaa kaa karibu na ndege...We unataka kupaa unakuwa rafiki wa Nyangumi...UNAZAMISHWA SASA HIVI!!

Tangu nianze kukaa na watu Positive I have changed a lot...Nikiwaza jambo wanauliza HOW DO WE ACHIEVE THIS na sio FULANI ALIWAHIFANYA HII AKAFELI..
Ikikusaidia Chukua..
KILL ALL NEGATIVE PEOPLE AROUND YOU kama unataka kufikia Malengo Makubwa, I will be ur Lawyer at the Court na mwambie Hakimu nilikutuma mimi!

Akamaliza.

0 comments:

Post a Comment

.

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!