2 June 2015

Hii ni moja ya video iliyo rekodiwa na mwana dada Hoyce Temu, video hii imepigwa maeneo ya Tandika, Wilaya ya Temeke Mkoa wa Dar es Salaam.

Mtangazaji huyu aliweza kuwatembelea watumiaji wa madawa ya kulevya na kushuhudia jinsi wanavyo jidunga sindano, kwa kutafuta mishipa ya damu, haswa maeneo ya mikononi na miguuni. Na ikishindikana kupatikana basi ufikia hata kujidunga kwenye maeneo ya shingoni ambako mishipa ya damu ipo karibu sana na Moyo na wenyewe wanakiri kuwa ni hatari na dawa upanda kwa haraka zaidi.

Wachache walio hojiwa wanaomba kama ikiwezekana basi wapatiwe msaada ili waweze kuacha kutumia haya madawa.

Je wewe una maoni gani kwa watumiaji wa madawa ya kulevya, je unao uwezo wa kuwatembelea maeneo yao na kuwapa ushauri nasaha au kuwaelekeza maeneo ambayo wanaweza kupata msaada ili waepukane na haya matumizi ya madawa ya kulevya!?

Video hapa chini inajieleza.


0 comments:

Post a Comment

.

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!