12 October 2014

Walimu Wa Madrsa Na Maimamu Wa Misikiti Wanatakiwa Kuwa Na Tahadhari Na Utapeli Huu.

Kuna mama mmoja wa kiarabu mwenye jina la Nuraisha Jamal Namba Ya Simu 0716 33 61 33 alipiga simu kwa mwalimu wa Madrasat Da'wat Islamiyah iliopo Kigogo Dar es Salaam kwa ustadh Hassan Ndaro kwenye namba hii 0719 11 49 55 na kumwambia ofisi yake imepokea maombi yao ya siku nyingi ya ujenzi wa Madrsa na maombi yamekubaliwa na waende Mororgoro wakachukue pesa zisizo pungua Tsh milioni 40.

Walimu wale wakajikusanya na wakaenda walimu wawili uko Morogoro na kufikia jilani na benki ya NBC mjini Morogoro .
Walipo mpigia simu yule mama akawaambia kuwa gharama za ujenzi zimepanda kwa hiyo bora waongee na mkubwa wake wa kazi ili awaongezee pesa. Akawapa namba ya simu ya huyo aliyeitwa mkubwa na wakaongea naye na akawapa ahadi ya kuwaongezea Tsh milioni 34, na akawata waende Tawa la benki NBC pamoja na nyaraka zao na wamkabidhi karani aliyewaelekeza.

Walipoingia benki na kuonana na yule karani, akawaambia kuwa nyaraka zina mapungufu. Na ili awasaidie akawataka watoe Tsh laki mbili (Rushwa), na nyaraka  zikikamilishwa zitatumwa kwa fax kwa wahusika. Yule karani akawataka wazitume zile pesa kwa Yule mama wa Kiarabu kwa kutumia tigo pesa. Kisha wakatakiwa warudi zao Dar es Salaam na kuagizwa waende benki ya NBC Magomeni siku ya Ijumaa ya tarehe 26/09/2014 na wamuone mtu mwingine mwenye namba 0789 079 539 na atawapa hela zao kutoka account namba 2017 4285 8422.
Walipokwenda kwa Yule mtu walie agizwa kwake naye akawadai rushwa ya Tsh laki mbili na wazitume kwa yule yule mama wa Kiarabu.
Wale Waalim kufikia hapo wakawa wanazungurushwauku mara kule na hawajapewa hela walizo ahidiwa na wala hawajarudishiwa pesa zao walizotoa ili kuwezesha kupata huo msaada kwa ajili ya madrasa zao.

Maelezo haya ni kwa mujibu wa Mwalimu mkuu wa Madrasat Da'awah Sheikh Ramadhani Ndaro anapatikana kwa namba hizi 0755 26 62 90.

Tukio kama hili limeikuta Madrasat Shaadhifyyah ya Ustadh Hashim mwenye namba 0783 53 74 74, iliyopo maeneo ya Buguruni kwa Makukula. Nao walitakiwa watoe laki mbili ya fax ili kufanikisha huo msada , walipokosa laki mbili huyo mama akawaambia yeye atatoa laki moja na wao watoe laki moja. Na wakipokosa na kuanza kupata wasi wasi akawaambia waende ofisini kwake Morogoro kama alivyosema mmoja wa wanafunzi ya Madrasah hiyo Bwana Suleiman Ally mwenye namba 0714 35 32 22.

Kwa Maelezo Zaidi Wasiliana Na Ustadh Musa Kileo kwa namba hii 0754 39 39 95 au kwa email hii: Kileomja@gmail.com

0 comments:

Post a Comment

.

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!