Showing posts with label Mastar. Show all posts
Showing posts with label Mastar. Show all posts

15 June 2012


Wema akiwa ndani ya mjengo wake.

Kwa mujibu wa chanzo kisicho na shaka ambacho ni mmoja wa mashosti wa Wema, wamedai nyumba iliyosemekana ni ya Wema Sepetu anayotarajia kuhamia hivi karibuni ipo Mtaa wa Bwawani, Kijitonyama jijini Dar es Salaam sio ya kwake.

MADAI MABICHI
Kikifichua mambo mazito nyuma ya pazia, chanzo hicho kilidai kuwa watu wanaoijua ishu hiyo kiundani walipigwa na butwaa waliposikia Wema anamiliki mjengo huo wa kifahari huku wao wakielewa vingine.
“Ninavyojua ile nyumba siyo yake bali amepanga tu,” kilidai chanzo hicho na kuongeza:
“Aisee! Nimeshangaa kusikia Wema kanunua lile jumba wakati mchakato wa kwanza wakiwa na madalali walikuwa wakitafuta nyumba ya kupanga.
“Kusema kweli jambo lililonishangaza ni kuwa mpaka mchakato wa mwisho unafanyika kuhusiana na nyumba hiyo ni kwamba Wema alikuwa anaipangisha na siyo kuinunua.”

SIKIA HILI JIPYAAA
Wakati tukisikiasikia hayo, tukaletewa lingine jipya na sosi mwingine kuwa Wema alipewa jumba hilo lililokuwa likimilikiwa na mama Ngoma ili amalizie kurekodi filamu yake mpya ya The Superstar.
“Si mnakumbuka alivyofanya juzikati kwa kuvishwa pete ya uchumba na Mwinyi wa Machozi kumbe alikuwa anarekodi filamu, ndiyo hivyohivyo kwa hili jumba, kama hamuamini mtaona baadaye.
“Wewe angali vizuri hizo picha, ni za filamu kabisa kwani kipande cha hiyo muvi kinamtaka aonekane akiishi maisha ya kistaa sana. Wewe nyumba gani umetenga mpaka chumba cha kuzungumza na vyombo vya habari?” alihoji sosi huyo.

UTATA
Wakati mambo yakizidi kuwa mengi, kikaibuka chanzo kingine kikidai kuwa si kweli kwamba mjengo huo unamilikiwa na mama Ngoma bali ni ya Mwarabu fulani.
Baada ya kuambiwa vitu kibao kuhusu jumba hilo, Ijumaa lilianza kusaka ukweli ili kujibu maswali ya mashabiki wa Wema.

HUYU HAPA MENEJA WAKE
Mtu wa kwanza kuzungumza na Ijumaa ni meneja wa Wema, Martin Kadinda ambaye alikiri Wema kununua nyumba hiyo lakini si kwa Sh. milioni 400.
“Unajua huyo anayesema kuwa Wema amepanga siyo kwamba anakosea ila anachelewa kujua mambo.
“Ni kweli kabisa mara ya kwanza Wema alikuwa anataka kupanga nyumba hiyo lakini baadaye alikaa chini na mwenye nyumba na kukubaliana kufanya biashara ya kumuuzia lakini si kwa Sh. milioni 400,” alisema Martin.

MILIONI 400 KIVIPI?
Akifafanua fedha hizo zinazodaiwa kununulia mjengo huo, Martin alisema:
“Hiyo milioni 400 ni thamani ya nyumba na vitu vyote vya ndani. Siyo bei iliyonunuliwa.”

Kwa habari zaidi soma hapa GLOBAL PUBLISHERS INFO

10 June 2012

 Lisebule heheyaaaaa
 Maishallah hongera 
 Tenaaaa


Mmeona eeeh
 Wema,Zamaradi na Snura

 Shurti kwa ji Kaunta 
 Mbona kama.....au hii dera tu,hahahahahahahahaha
 Hii ni kwa ajili ya kwendea sokoni hahahaha,msinisonye jamani
 Ndiga zake hizi hapa
Yes ni maeneo ya Kijitonyama ndipo anapoishi my gal Wema sepetu,ndio hata kama amepanga lakini si ndio nyumbani kwake jamani,hahahahahah haya basi mtuonyeshe na nyie za kwenu hahahaha mmenuna eeeeh .
Kwa Picha zaidi ingia hapa Chini
DJ CHOKA BONGO STAR LINK

4 June 2012

                                                                 Musa Mateja na Shakoor Jongo
WEMA Isaac Sepetu ‘Pedeshee Mwanamke’, amefanya kufuru mpya baada ya kuvuta mkoko wa maana wenye thamani ya Sh. milioni 38 na kumpa mama yake, Miriam Sepetu ule usafiri aliokuwa akitumia wa Toyota Lexus Harrier.
Wema ambaye ni tishio katika filamu za Kibongo na umodo alifanya tukio hilo Mei 25, mwaka huu kwa kile alichodai kuwa aliona mama yake anateseka na usafiri kwani siku chache gari la mzazi wake huyo alilokuwa akitumia lilipata hitilafu.
AINA YA GARI
“Ni Toyota Mark X. Muda mrefu nilipanga kununua gari la kifahari lakini kitendo cha kuharibika kwa gari la mama kimechochea mimi kununua gari hili,” alisema Wema.
ANAPATA WAPI JEURI?
Ni kitambo sasa, Wema kama ilivyo kwa Jacqueline Wolper, amekuwa hana shida ndogondogo kwa kuwa mkwanja anao wa kutosha na kwa mujibu wa rafiki yake wa karibu, amenunua gari hilo ili kuwathibitishia kuwa fedha siyo tatizo kwake kwani ana ‘mnene’ anayemuwezesha.
Habari kwa Hisani ya: www.globalpublishers.info

3 June 2012



 Fiona mbwa wa Wema Sepetu Apimiwa Magauni kwa Fundi Cherehani
Wema alitoa maelekezo kwamba anataka Fiona ashonewe nguo za rangi mbalimbali ambazo yeye anazo ili wakitoka wote wawe wanamechisha.

 Wema kwa kweli kitendo hiki kwa imani tu ya dini ni kufuru uliyoifanya,sikuingilii katika maamuzi yako lakini nikiwa na kashibiki wako,na ndugu yako katika imani ya dini,kwa kweli kitenbdo hiki sio kizuri kabisa.

Wema kitendo ulichafanya ni kufuru kwa mwenyezimungu,hebu kaa na ujiulize kuna watoto wangapi vijini ambao hawana hata nguo za kuvaa wewe ukamshonee mbwa  ambaye ameumbwa Mwenyezimungu kuishi mazingira ya kutovaa nguo,tena unajifaragua eti oooh tukitoka tuwe tumevaa sare sare hakika huo ni ulimbukeni wa akili.

Halafu kama mnataka kuiga hao watu maarufu wa huko mbeleni sidhani kama wao wanakwenda na mambwa katika sherehe kama alivyofanya huyo mjengezi mwenzio Irene alipombeba mbwa katika sherehe ya watu,nina waapia laiti sherehe ingekuwa ya kwangu yule mbwa asingeingia kabisa.

Wema wewe ni msichana muelewa na uliyepitia maisha mazuri,usiwe limbukeni na mtu mkosa maadili kwa kumuita mbwa eti ndio mtoto wako.Igizeni vitu vizuri na sio kuiga mambo ya ajabu,au ndio kutaka kuonekana mnaandikwa kila siku katika magazeti ya rangi rangi bila ya kupewa kitu chochote.

Basi hao watu maarufu wenzenu wakiandikwa wanalipwa na sio kuandikwa tu kama mnavyofanya nyie,baada ya nyie mlipwe,nyie ndio mnatoa pesa huu ni ukosefu wa ufahamu kabisa.

picha:global publisher

2 June 2012





Wema na Nasib (diamond)enzi za penzi la shatashata, ambalo sasa limebaki historia

MWANAMUZIKI nyota
Tanzania, Diamond amesema kwamba kufanya kwake vizuri katika mahojiano
ya lugha ya kiingereza aliyoyafanya  kwenye jumba la Big Brother hivi karibuni, nchini
Afrika Kusini, ni kutokana na mafunzo mazuri ya kuzungumza lugha hiyo,
aliyopewa na mpenzi wake wa zamani, Wema Sepetu.


Diamond ameyasema
hayo katika kipindi cha XXL cha Clouds Radio- baada ya
kuulizwa siri ya kujiamini kwake kuzungumza vema Kiingereza bila kitete
alipokuwa akihojiwa BBA.


amesema anamshukuru mama yake mzazi na mpenzi wake wa zamani
"Namshukuru sana
mama yangu mzazi kwa kunisomesha, lakini pia namshukuru Wema Sepetu kwa kweli alinisaidia sana wakati nipo naye kunifundisha
kuzungumza Kiingereza kwa kujiamini,"alisema Diamond.


Diamond anakuwa
msanii wa pili kuzungumza hadharani kunufaika na lugha ya Kiingereza
kutoka kwa Wema, baada ya marehemu Steven Kanumba naye kuwahi kusema
hapo awali, alisaidiwa mno na Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006 kunyoosha
lugha huyo.
Kwa hisani ya Bongostarz.blog/this day magazine
Kutoka tmark-turn hakika Wema wewe ni mwema kama jina lako lilivyo na pia ni mke mwema isipokuwa huna bahati na hawa watu wanaoitwa wanaume,inshallah mwenyezimungu atakujalia mume mwenye kheri na wewe. 

.

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!