1 June 2014


Edson Cholbi do Nascimento Pele mtoto wa aliyekuwa mchezaji gwiji wa kusakata soka duniani Pele na kipa wa zamani amahukumiwa kifungo cha miaka 33 jela


Edinho mwenye umri wa miaka 43 aliyekuwa chezaji mpira wa miguu mstaafu kwenye timu ya Santos amahukumiwa kwenda jela miaka 33 kwa makosa ya ufisadi na fedha chafu zinazotokana na madawa ya kulevya.

Edinho kwa mara ya kwanza alikamatwa mwaka 2005 na alitumikia adhabu ya kifungo kwa makosa ya kusafirisha madawa ya kulevya, pamoja na kuwa na mahusiano na wauza madawa ya kulevya mjini Santos.

Mtoto huyo wa mfalme wa soka, Pele alikuwa akichezea club ya Santos nafasi ya golikipa mwishoni mwa miaka ya 90.

Edinho, ambaye kwa sasa anafanya kazi ya ukocha akifundisha magolikipa wa timu ya Santos, habari zinasema kuwa yeye ni mtumiaji mkubwa wa madawa ya kulevya lakini amekana madai ya kuhusika na uhuzaji na kufanya biashara ya kuuza madawa.

Vyombo vya habari vya Brazil havijaweza kumuhoji Edinho, ambaye jina lake halisi ni  Edson Cholbi do Nascimento. Anatarajiwa ya kukata rufaa.

Edinho ni mtoto wa tatu wa Pele kwenye ndoa yake ya kwanza Pele alipohamia New York kuchezea Cosmos Edinho alikuwa na miaka tano tu.


 Mwaka 1995 Edinho ndiye aliyekuwa golikipa wakati timu ya Santos ilipocheza fainali ya ligi ya Brazil, dhidi ya Botafogo .

Pele aliwahi kwenda kumtembelea motto wake, alipokuwa jela mwaka 2006, na alisema: "Mungu akipenda, haki itapatikana, Hakuna hata chembe ya ushahidi dhidi ya mwanangu"


0 comments:

Post a Comment

.

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!