29 May 2014


Wasichana wawili wa kihindi waliopatikana wakiwa wananing'inia kwenye mti katika jimbo la Uttar Pradesh, walikuwa wamebakwa kisha wakanyongwa.

Polisi wanasema kuwa mwanamume mmoja amekamatwa kuhusiana na mauaji hayo huku polisi watatu wakiachishwa kazi kwa kutosajili kesi hiyo iliporipotiwa kuwa wasichana hao walikuwa wametoweka, kabla ya kupatikana wakiwa wameuawa.

Wasichana hao walipatikana katika wilaya ya Badaun na wanadhaniwa kuwa na umri mdogo kuanzia 13 hadi 15

Ubaguzi dhidi ya wanawake umekita mizizi katika jamii nyingi nchini India.

Visa vya dhuluma za kingono vimeendelea kukithiri nchini India tangu mwaka 2012 ambapo msichana mmoja alibakwa na genge la vijana hadi kufa

Serikali ililazimika kuweka sheria kali kwa wanaopatikana na hatia ya kutenda vitendo vya dhuluma za kingono baada ya maandamano kufanyika kote nchini kufuatia shambulizi hilo.

Polisi mmoja aliambia BBC kuwa wasichana hao walikuwa na uhusiano wa kifamilia na walipatwa wakiwa wananing'inia kwenye mti kijiji cha Badaun mnamo siku ya Jumatano.

Alisema kuwa polisi wanawasaka wanmaume wawili waliowabaka wasichana hao na kisha kuwanyonga.

Wasichana hao walichomwa kuambatana na tamaduni za maziko ya kihindi Jumatano.

Polisi wanasema wanachunguza ambavyo wasichana hao walipotea, kubakwa na kisha kuwekwa kwenye mti.

0 comments:

Post a Comment

.

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!